Job 18:5-10


5 a“Taa ya mwovu imezimwa,
nao mwali wa moto wake umezimika.

6 bMwanga hemani mwake umekuwa giza;
taa iliyo karibu naye imezimika.

7 cNguvu za hatua zake zimedhoofishwa;
shauri lake baya litamwangusha.

8 dMiguu yake imemsukumia kwenye wavu,
naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.

9 eTanzi litamkamata kwenye kisigino;
mtego utamshikilia kwa nguvu.

10 fKitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake;
mtego uko kwenye njia yake.
Copyright information for SwhKC