Job 18:5-10
5 a“Taa ya mwovu imezimwa,
nao mwali wa moto wake umezimika.
6 bMwanga hemani mwake umekuwa giza;
taa iliyo karibu naye imezimika.
7 cNguvu za hatua zake zimedhoofishwa;
shauri lake baya litamwangusha.
8 dMiguu yake imemsukumia kwenye wavu,
naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
9 eTanzi litamkamata kwenye kisigino;
mtego utamshikilia kwa nguvu.
10 fKitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake;
mtego uko kwenye njia yake.
Copyright information for
SwhKC